Waliosombwa na maji Myanmar waendelea kuokolewa

0
2256

Waokoaji nchini Myanmar wanaendelea na zoezi la kuwaokoa watu waliosombwa na maji baada ya bwawa moja kubwa nchini humo kupasuka na maji yake kusambaa hovyo hadi katika makazi ya watu.

Zaidi ya watu Sitini Elfu wamelazimika kuyahama makazi yao huku vijiji vipatavyo mia moja vikiwa vimefunikwa na maji.
Habari kutoka nchini Myanmar zinasema kuwa watu wawili hawajulikani walipo baada ya kusombwa na maji hayo.

Nchi ya Myanmar katika siku za hivi karibuni imekuwa ikishuhudia mvua kubwa iliyosababisha mafuriko na kufanya kingo za mito mingi kupasuka.
Idara ya hali ya hewa nchini Myanmar imetoa taarifa inayosema kuwa mvua hizo ambazo ni za msimu zitaendelea kunyesha kwa siku kadhaa.