Dkt. John Magufuli na Samia Suluhu wateuliwa kugombea muhula wa pili

0
341
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mgombea Mwenza Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma mara baada ya kuchukua fomu za kugombea kwa muhula w apili.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kumteua Rais Dkt. John Magufuli kugombea Urais wa Tanzania na Mama Samia Suluhu kugombea nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

NEC imetoa taarifa hiyo muda mfupi baada ya wagombea hao kurejesha fomu katika ofisi za taasisi hiyo zilizopo Ndejengwa jijini Dodoma.

Akizungumza mara baada ya kupokea fomu hizo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu, Semistocles Kaijage amesema kuwa wagombea hao wamekidhi vigezo vya kisheria, na amewatakia heri katika mchakato mzima wa uchaguzi.