Yanga yaomba kujitoa kombe la Kagame

0
1923

Uongozi wa klabu ya Yanga umeliandikia barua shirikisho la soka hapa nchini TFF  kuwaomba kujitoa katika mashindano ya Kagame Cup yanayotarajiwa kuanza June 28 mpaka Julai 13 mwaka huu jijini Dar Es Salaam.

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten amesema sababu za msingi zilizofikia Yanga kuandika barua hiyo ni kufanya maandalizi ya michunao ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo watacheza na Gor Mahia FC ya Kenya, Julai 18 jijini Nairobi nchini Kenya.

Kutokana na muingiliano wa ratiba ya Kagame na CAF, Yanga wameona ni vema kuwapatia wachezaji wao mapumziko ili kuwapa fursa ya kujiandaa vizuri kuelekea mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya tatu baada ya kucheza na USM Alger pia Rayon Sports ya Rwanda.

Enock Bwigane
08 Juni 2018