Vettel ajitapa kushinda

0
1979

Dereva wa kampuni ya Ferari, -Sebastian Vettel amesema kuwa bado ana nafasi ya kushinda taji la mbio za langalanga msimu huu licha ya kuachwa kwa tofauti ya alama hamsini na mpinzani wake mkubwa Lewis Hamilton.

Hamilton amejiweka katika nafasi nzuri ya kushinda taji la tano la mbio za langalanga baada ya kuibuka kinara katika michuano ya Russian Grand Pri iliyofanyika mjini Sochi.

Ushindi huo unamfanya Hamilton kufikisha alama 306 katika nafasi ya kwanza kwenye msimamo, huku Vettel akiwa katika nafasi ya pili akiwa na alama 256.

Vettel amesema kuwa anajua si kazi rahisi kupindua matokeo hayo lakini atafanya kila analoweza kuwashangaza wengi mwisho wa msimu.

Mpaka sasa yamebaki mashindano matano kukamilisha msimu yatakayofanyika katika nchi za Japan, Marekani, Mexico, Brazil na Abu Dhabi.