Timu ya Los Angeles yafungwa katika ligi ya kikapu Marekani

0
925

Ligi ya kulipwa ya mpira wa kikapu nchini Marekani ya Nba imendelea na kuchezwa michezo saba.

Los Angeles Lakers wakiwa ugenini wamekiona cha moto baada ya kunyukwa alama 108 kwa 86 na Minasota Timberwolves ambao wamepata ushindi wa 19 msimu huu wakati Lakers wakipoteza mchezo wa 19.

Katika matokeo mengine Miami Heat wamenyukwa alama 106 kwa 82 na Atlanta Hawks wakati Washngton Wizards wakiinyuka Oklahoma City Thunder alama 116 kwa 98 na Charlote Hornets wameilaza Phonix Suns alama 119 kwa 113.

Los Angeles Clippers wameshinda  nyumbani kwa kuinyuka Orlando Magic alama 106 kwa 96 wakati Indiana Pecers wakishindwa kuhimili vishindo vya Toronto Raptors na kula mweleka wa alama 121 kwa 105 huku Brooklyn Nets wakiinyuka Chicago Bulls Al.