Timu sita kumenyana ligi kuu

0
1014

Timu ya Alliance fc ya Mwanza itateremka dimbani kuvaana na RUVU Shooting kwenye uwanja wa nyamagana mkoani Mwanza.

Biashara United ya Mara inawaalika wagonga nyundo wa jiji la Mbeya – Mbeya City fc kwenye uwanja wa kumbukumbu Karume mjini Musoma huku.

Nayo timu ya  Singida United wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa NamfuA mjini Singida wanawakaribisha Coastal Union ya Tanga huku Kagera sugar wakikipiga na Mbao fc.

Kwenye mchezo pekee uliochezwa hapo Januari Mosi ,timu ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni (Kmc) imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa nunge dhidi ya kikosi cha African lyon katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam .

Kwa ushindi huo, Kmc inafikisha alama 25 baada ya kushuka dimbani mara 19 ambapo inapanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu kutoka nafasi ya tisa iliyokuwepo kabla ya mchezo wa January Mosi.