Stars mazoezini AfrikaKusini

0
2243

Timu ya Taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars) inaanza mazoezi leo Novemba saba kwenye kambi yake iliyoweka huko mjini Bloomfontein nchini Afrika Kusini ikiwa ni sehemu ya kujiwinda na mchezo wa kufuzu kwa fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya wenyeji Lesotho.

Kikosi cha Stars kiliwasili nchini Afrika Kusini Novemba sita mwaka huu kikiwa na wachezaji wanaocheza soka hapa nchini ambao wataanza mazoezi kabla ya kuungana na wale wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi katika kambi hiyo ya Afrika Kusini.

Taifa Stars watakuwa wageni wa Mamba wa Lesotho Novemba 18 mwaka huu katika uwanja wa Setsoto mjini Maseru kwenye mchezo muhimu wa Kundi L ambapo inahitaji ushindi ili kufuzu kwa fainali za AFCON kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 38.