Stars kuifuata Cape Verde usiku wa leo

0
1922

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka usiku wa leo Oktoba Tisa kuelekea nchini Cape Verde kwa ajili ya mchezo wa kuwania kushiriki michuano ya mataifa ya Afrika dhidi ya timu ya taifa hilo.

Katika safari ya Stars, kiungo Frank Domayo ndiye mchezaji pekee ambaye anaweza kuukosa mchezo huo kutokana na kukabiliwa na majeraha ambayo aliyapata kwenye siku ya pili ya mazoezi ya Taifa Stars.

Meneja wa  timu hiyo Daniel Msangi amesema kuwa wachezaji wengine ambao waliumia wakati wakizitumikia klabu zao wana uwezekano mkubwa wa kuwepo kwenye safari ya leo usiku tayari kwa mchezo huo utakaochezwa siku ya Jumamosi Oktoba 12.

Msangi ameongeza kuwa mazoezi ya Stars kuelekea kwenye pambano hilo yameimarika hasa baada ya baadhi ya wachezaji wanaocheza soka nje nchi kujumuika na kikosi hicho.