Simba na Azam kuvaana fainali ya michuano ya Mapinduzi

0
1059

Timu za Simba na Azam Fc zitakutana fainali hapo Januari  13 kuwania ubingwa wa michuano ya kombe la mapinduzi baada timu hizo kutinga fainali mchezo utakaofanyika katika dimba la Gombani kisiwani Pemba .

Simba wametinga fainali baada ya kuifunga timu ya Malindi kwa mikwaju ya penati mitatu kwa  moja katika mchezo uliochezwa Januri 11.

Mabeki Yussuf  Mlipili, Mghana Asante Kwasi na kiungo Mohammed ‘mo’ Ibrahim waalifungia  Simba penalti zao huku beki mpya, Zana Coulibaly kutoka Burkina Faso alikosa penati kutokana na kupiga mpira  juu.

Kwa upande wa Malindi, Abdulswamad Kassim pekee alifunga penalti yake, huku Ali Kani, Muharami Issa na Cholo Ali walikosa penati wote.

Bingwa mtetezi wa Michuano ya Kombe la Mapinduzi, Azam Fc wametinga kwa kishindo fainali ya michuano hiyo kwa kuishushia timu ya KMKM kipigo cha mabao matatu kwa bila kwenye mchezo wa nusu fainali uliochezwa kwenye dimba la Aman Mjini Unguja.

Mabao ya nahodha Aggrey Morris kwenye dakika ya 9, Salu Aboubakar dakika ya 62 na Obreyt chirwa aliyefunga bao la tatu kwenye dakika ya 82 yametosha kuipeleka Azam Fc kwenye fainali ya tatu mfululizo ya michuano hiyo.

Bingwa wa michuano hiyo atajinyakulia kikombe pamoja na kitita cha shilingi Milioni 15 huku makamu bingwa akijizolea kitita cha shilingi milioni 10.

Matangazo yote katika michuano hiyo yatakujia moja kwa moja kupitia Tbc Taifa.