Timu ya Simba ya Tanzania leo inashuka katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuivaa Js Soura ya Algeria kwenye mchezo wa Ligi ya mabingwa wa Afrika huku ikiwa na matumaini ya kupata ushindi mnono.
Kocha wa Simba Patrick Aussems akizungumza Januari 11 amesema kuwa amefanya maandalizi mazuri ya timu na kwamba ana imani na timu yake kufanya vizuri katika mchezo huo .
Amesema wanawaheshimu wapinzani wao hao kwani wana imani kuwa nao wamejiandaa vyema kukabiliana nao hivyo amewajenga wachezaji wake vizuri katika kupambana.
Simba ambayo ipo kundi D pamoja na timu za Al Ahly ya Misri,As Vita ya Congo ya Drc na Js Saoura ya Algeria itakuwa inashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu ya kuitoa timu ya ya Nkana Rangers ya Zambia kwa mabao matatu kwa moja na kufanikiwa kutinga hatua ya makundi.