Simba kuwavaa JS Soura ya Algeria katika hatua ya makundi

0
1018

Timu ya Simba ya Tanzania leo inashuka katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuivaa Js Soura ya Algeria kwenye mchezo wa  Ligi ya  mabingwa wa Afrika huku ikiwa na matumaini ya kupata ushindi mnono.

Kocha wa Simba  Patrick Aussems akizungumza  Januari 11  amesema kuwa amefanya maandalizi mazuri ya timu na kwamba ana imani na timu yake kufanya vizuri katika mchezo huo .

Amesema wanawaheshimu wapinzani wao hao kwani wana imani kuwa nao wamejiandaa vyema kukabiliana nao hivyo amewajenga wachezaji wake vizuri katika kupambana.

Simba ambayo ipo  kundi  D pamoja na  timu za Al Ahly ya Misri,As Vita ya Congo ya Drc na Js Saoura ya Algeria itakuwa inashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu ya kuitoa timu ya  ya Nkana Rangers ya Zambia  kwa mabao matatu kwa moja na kufanikiwa kutinga hatua ya makundi.