Timu ya Taifa ya soka ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) imerejea nchini ikitokea nchini Botswana baada ya kutwaa ubingwa wa soka kwa ukanda wa Tano wa Afrika.
Timu hiyo iliifunga Angola penati sita kwa tano katika mchezo wa fainali.
Serengeti Boys wamelakiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe ambaye amewapongeza wachezaji hao kwa ushindi walioupata.
Timu ya Serengeti Boys kwa sasa inaanza kujiandaa na michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 itakayofanyika mwaka 2019 nchini.