Serena atozwa faini Dola 17,000 za Marekani

0
2250

Nyota wa mchezo wa Tennis duniani mkongwe Serena Williams ametakiwa kulipa faini ya dola za Marekani 17,000 sawa na zaidi ya Shilingi milioni 38 kwa makosa mbali mbali aliyoyafanya usiku wa juzi jumamosi Septemba 08 kwenye mchezo wa fainali ya mashindano ya wazi ya marekani (US OPEN) dhidi ya Mjapani Naomi Osaka.

Faini hiyo inahusu makosa kadhaa ikiwemo lile la kumuita mwamuzi wa mchezo huo muongo na mwizi wa alama zake, kupokea maelekezo kutoka kwa kocha wake wakati mchezo ukiendelea kinyume cha sheria za mchezo huo pamoja na kuvunja ‘racket’ yake kwa makusudi wakati wa mchezo.

SERENA alionekana kujawa na jazba hasa baada ya muamuzi Umpire kumkata alama katika mchezo huo dhidi ya Naomi ambapo alipoteza kwa kipigo cha seti mbili kwa bila za ushindi wa 6-2 na 6-6 hivyo kumfanya Naomi kushinda Grand Slam yake ya kwanza kutoka kwenye mikono ya aliyekuwa Role Model wake.

Ushindi wa Naomi mbele ya Serena unamfanya kupanda katika viwango vya ubora kutoka nafasi ya 19 aliyokuwepo awali hadi nafasi ya 7 huku nyota wa zamani wa mchezo huo kutoka nchini Japan Kimiko Date akisema Mjapan mwenzake huyo anastahili kuwa nambari moja kwenye viwango vya ubora kwa sasa.