Samatta aendelea kufanya vizuri Genk

0
2555

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta amefunga mabao matatu – Hat Trick katika mchezo ambao timu yake ya KRC Genk imeibuka na ushindi wa mabao matano kwa mawili dhidi ya Brondby IF ya Denmark katika mchezo wa kwanza wa hatua ya mwisho wa mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Europa.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Luminus mjini Genk, Samatta amefunga mabao yake katika dakika za 37, 55 na 70 wakati mabao mengine ya Genk yamefungwa na mshambuliaji Mbelgiji, Leandro Trossard kwa penalti dakika ya 45 na Ushei aliyefunga la mwisho katika dakika ya 90.

Genk sasa watatakiwa kwenda kuulinda ushindi wao katika mchezo wa marudiano ugenini, agosti 30 kwenye uwanja wa Brondby na endapo watapata ushindi wa jumla watatinga moja kwa moja hatua ya makundi ya michuano hiyo.