Rooney amtetea Mourinho

0
1950

Mshambuliaji wa zamani wa timu ya Manchester United, – Wayne Rooney amesema kuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho sio mlengwa namba moja kwenye kufanya vibaya kwa timu hiyo bali wachezaji wake wanatakiwa kupambana.

Mourinho amekuwa na wakati mgumu baada ya Manchester United kuwa  na mwanzo mbaya  kwenye ligi kuu ya England na imefika wakati kuzushiwa kuwa anaweza kutimuliwa kazi.

Rooney amesema kuwa anajua fika kuwa  Mourinho yupo kwenye wakati mgumu hivi sasa lakini wachezaji lazima wasimame imara na kuifanya kazi yao ipasavyo.

Nyota huyo anayecheza soka nchini Marekani kwa sasa kwenye klabu ya D.C United ameongeza kuwa kocha anaweza kufanya kila kitu lakini atakuwa nje ya uwanja,  sasa kazi inabaki kwa wachezaji ambao ndio wanashuka dimba hivyo nao lazima waonyeshe nini wanafanya.