Nyota wa Liverpool wawania tuzo za wachezaji bora Afrika

0
955

Nyota wawili wa Liverpool Mohamed Salah raia wa Misri na Sadio Mane raia wa Senegal wameingia kwenye orodha ya wachezaji watatu wa mwisho wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa afrika zitakazotolewa wiki ijayo jijini dakar, Senegal.

Wachezaji wote wawili wamekuwa na kiwango kizuri mwaka uliopita wakiitumikia klabu yao ya Liverpool na timu zao za taifa ambapo Salah anatetea taji hilo kufuatia kuibuka kidedeaa mwaka jana.

Mwaka jana Salah alivunja rekodi ya upachikaji mabao kwenye ligi kuu ya Egland baada ya kupachika kimiani mabao 38 na kuifikisha klabu yake kwenye fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya.

Kwa upande wake Sadio Mane aliyeshika nafasi ya pili kwenye tuzo za mchezaji bora za mwaka jana, naye alikuwa na kiwango kizuri lakini akiwa nyuma ya salah kwenye takwimu za upachikaji mabao kwenye klabu yao huku wakiunda safu nzuri ya ushambuliaji wakiwa sambamba na mbrazil – roberto firmino.

Mchezaji anayekamilisha idadi ya wachezaji watatu kwenye kinyang’anyiro hicho ni mshambuliaji wa Arsenal na timu ya Taifa ya Gabon – Pierre Emerick-Aubameyang ambaye ni mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka 2015.

Nyota huyo aliifungia Arsenal mabao 10 msimu uliopita ukiwa ni msimu wake wa kwanza akitokea Borussia Dortmund ya Ujerumani ambapo kwa mwaka jana peke yake, ukiwa ni msimu wa mwaka 2018/2019 amefunga mabao 14.