Nurmagomedov sasa amtaka Myweather

0
1910

Bingwa wa uzani wa juu katika mchezo wa masumbwi Khabib Nurmagomedov wa Russia amesema yupo tayari kuzichapa na mbabe wa Kimarekani Floyd Myweather muda wowote atakapohitajika kufanya hivyo.

Nurmagomedov amesema kuwa anataka kushinda kitu alichoshindwa mpinzania wake Conor McGregor na kuongeza kuwa siku zote mfalme wa pori ni mmoja tu.

Mapema mwezi huu Mrussia huyo alimnyuka Mcgregor ambaye alikuwa hajapanda ulingoni katika uzani wa juu tangu alipotwangwa na Myweather mwezi Agosti  mwaka  2017 na kutanua wimbi la ushindi katika rekodi zake kufikia mapambano 27 huku akiwa hajapoteza pambano hata moja.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa  instagram,  Nurmagomedov ameonekana akisema kuwa ni wakati wa kupigana na Myweather huku Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Mayweather Promotions akisema kuwa wababe wawili ambao hawajapoteza pambano hata moja kwanini wasipigane.

Myweather hajapanda ulingoni tangu alimpomshinda McGregor kwa knockout katika raundi ya  kumi mwezi Agosti mwaka  2017 katika pambano ghali zaidi duniani huku akiwa na rekodi ya kucheza mapambano hamsini na kushinda yote.