Newcastle yafungwa katika uwanja wake wa nyumbani

0
1050

Timu ya Newcastle imepoteza mchezo wa nane kati ya kumi na moja waliyocheza ya ligi ya Uingereza kwenye uwanja wake wa nyumbani kwa msimu baada ya kukubali kipigo cha mabao mawili kwa bila kutoka kwa Manchester United.

Mabao ya Romelu Lukaku aliyetokea benchi katika dakika ya 64 na Marcus Rashford katika dakika ya 80 yanaifanya Manchester United kushinda mchezo wa nne mfululizo kwa mara ya kwanza tangu mwezi April mwaka 2018.

Manchester United sasa imeshinda michezo 68 kati ya 100 waliyocheza mwezi Januari na kuwa timu pekee iliyoshinda michezo mingi kwenye ligi kuu ya England kwa mwezi huo.

Katika matokeo ya michezo mingine Bournamouth wamelazimishwa sare ya mabao matatu kwa matatu na Watford wakati Westham United wakibanwa na kutoka sare ya mabao mawili kwa mawili na Brighton huku Crystal Palace wakiinyuka Wolves mabao mawili kwa bila na Chelsea wakishindwa kufurukuta nyumbani na kutoka suluhu dhidi ya Southampton.

Baade unachezwa mchezo mmoja wa ligi ya kandanda ya England ambapo vinara wa ligi hiyo Liverpool wenye alama 54 wanasafiri kuwafuata Manchester City wanaoshika nafasi ya tatu wakiwa na alama 47 mchezo utakaochezwa kwenye dimba la Etihad kuanzia majira ya saa tano kamili za usiku.