Mourinho ataka vyombo vya habari kumuheshimu

0
2545

Meneja wa Manchester United, – Jose Mourinho amevitaka vyombo vya habari vya England kumpa heshima kutokana na mafanikio yake kwenye soka la nchi hiyo.

Mourinho ameyasema hayo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari baada ya mchezo dhidi ya Tottenham Hot Spurs uliomalizika kwa kichapo cha mabao matatu kwa nunge ambapo amebainisha kuwa kichapo hicho si kitu kwani ana mafanikio makubwa kuliko kipigo ilichokipata timu yake hivyo aheshimiwe.

Mourinho amesema kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikimsakama haijalishi awe ameshinda ama amefungwa kwani akishinda vinamripoti kuwa ameshinda lakini timu yake imecheza vibaya.

Mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mourinho alienda moja kwa moja kwenye jukwaa la mashabiki wa Manchester United ambao walisalia uwanjani kwa dakika kadhaa baada ya kuisha kwa mchezo ambao walimpigia makofi wakionyesha kumuunga mkono.

Kwenye mchezo huo uliochezwa katika dimba la Old Trafford, mabao ya Man United yalifungwa na Harry Kane na Lucas Moura.

Kichapo hicho kimeipeleka Man United kwenye nafasi ya 13 ya msimamo wa ligi kuu ya England ikiwa na alama tatu baada ya michezo mitatu huku Tottenham ikikwea hadi nafasi ya pili nyuma ya vinara Liverpool.