Modric mchezaji bora wa mwaka wa Fifa

0
2423

Kiungo wa kimataifa wa Croatia,-Luca Modric ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Fifa baada ya kuwashinda Cristiano Ronaldo na Mohamed Salah.

Nyota huyo anayechezea Real Madrid aliisaidia klabu hiyo kushinda mataji matatu mfululizo ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya pamoja na kulisaidia taifa lake la Croatia kufika fainali ya kombe la Fifa la dunia.

Hii ni mara ya kwanza baada ya miaka kumi kupita tuzo kubwa duniani kunyakuliwa na mchezaji tofauti ya Ronaldo na Messi ambapo mara ya mwisho ilikuwa mwaka 2007 pale Mbrazil Ricardo Kaka aliposhinda tuzo ya Balon d’or.

Kwa upande wa goli bora la mwaka,  tuzo imeenda kwa Mohamed Salah wa Liverpool ambapo bao lake alilofunga dhidi ya Everton mwezi Disemba mwaka jana limeteuliwa kuwa goli bora la mwaka.

Ushindi huo hata hivyo umeibua mjadala hasa kutokana na ubora wa magoli mawili yaliyoshindwa likiwemo lile la Cristiano Ronaldo dhidi ya Juventus na lile la Gareth Bale dhidi ya Liverpool katika michuano ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya.

Tuzo ya kocha bora wa mwaka imeenda kwa Didier Deschamp wa Ufaransa wakati tuzo ya mchezaji bora wa kike ikienda wa Marta wa Brazil na tuzo ya mashabiki bora imeenda kwa mashabiki wa timu ya Taifa ya Peru.