Messi afanya kweli

0
2100

Lionel Messi amekua mchezaji wa kwanza kufunga goli la kwanza kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya msimu huu na pia kuwa mchezaji wa kwanza kufunga magoli matatu kwenye mchezo mmoja yaani Hat – Trick wakati timu yake ya FC Barcelona ilipoifunga PSV ya Uholanzi kwa bao nne kwa bila.

Messi ambaye kwa sasa ni nahodha wa miamba hiyo ya Catalunya, alianza kufungua milango ya PSV kwenye dakika 31 ya mchezo pale alipofunga kwa mpira wa adhabu ya nje ya kumi na nane na kuongeza magoli mengine mawili kwenye dakika za 77 na 87 na goli lingine la Barcelona lilitiwa kimiani na Ousmane Dembele.

Hadi sasa Messi amefunga Hat – Trick nane kwenye michuano hiyo ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya na kwa msimu huu tu amefunga magoli saba kwenye michezo sita aliyocheza.

Kwa ujumla Messi amefunga magoli 104 kwenye ligi ya mabinwa Barani Ulaya kwa michezo 14 aliyocheza akiwa na timu hiyohiyo ya Barcelona na kufikia rekodi iliyowekwa na nyota wa zamani wa Real Madrid, -Raul Gonzalez.