Mchezaji wa Azam ajiunga na timu ya Ismailia

0
944

Mshambuliaji wa timu ya Azam Fc, Yahya Zayed amejiunga na klabu ya Ismailia ya Misri kwa mkataba wa miaka mitatu.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Azam Fc, Jaffar Idd, amesema kuwa Zayed amejiunga na Ismailia bila ya kufanya majaribio zaidi ya kufanyiwa tu vipimo vya afya .

Zayed ambaye ni mchezaji  wa kimataifa wa Tanzania, mwenye umri wa miaka 20 amesaini mkataba huo kuitumikia Ismaili ambayo ni moja kati ya Klabu kongwe nchini Misri, na kuwa mchezaji wa pili wa Tanzania kucheza ligi kuu ya Misri, baada ya kiungo Himid Mao anayechezea Petrojet.

Nyota huyo pia anaungana na wachezaji wengine kutoka Namibia na Nigeria waliosajiliwa hivi karibuni kuboresha kikosi cha Ismailia  katika michuano mbalimbali ikiwemo hatua ya makundi ya ligi ya Mabingwa Barani Afrika ambapo wamepangwa katika kundi che.