Mashindano ya Taifa ya kikapu kufanyika tena Simiyu

0
1195

Baada ya mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu kufanyika kwa mafanikio mkoani Simiyu, uongozi wa shirikisho la mpira wa kikapu nchini TBF umeamua kuyapeleka tena mashindano hayo mkoani humo msimu ujao.

Rais wa TBF Phares Magesa amesema maandalizi yaliyofanywa na mkoa huo yameshawishi kuyarudisha mkoani Simiyu mashindano hayo mwakani.

Pia amesema mashindano hayo yamesaidia kuunda kikosi imara cha timu ya taifa ya mpira wa kikapu.

Mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu yaliyomalizika Jumapili Desemba 23 kwa timu ya mkoa wa Dar Es Salaam ya mchezo huo (The Dream Team) kutwaa ubingwa wa mashindano hayo baada ya kuinyuka timu ya mkoa wa Mwanza alama 78 kwa 75 kwenye mchezo wa fainali.