Mashindano ya Gofu Afrika kufanyikia Accra

0
2218

Timu ya Taifa ya mchezo wa gofu imeelekea nchini Ghana kushiriki mashindano ya Afrika kwa mchezo huo huku ikisema kuwa ipo tayari kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania.

Akikabidhi bendera ya taifa kwa timu hiyo, Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) – Alex Mkenyenge ameitaka timu hiyo kuwa na uzalendo.

Naye Rais wa Chama cha Gofu Tanzania kwa wanawake – Sophia Viggo pamoja na nahodha wa timu hiyo Madina Idd wamewashukuru wadau mbalimbali wa mchezo wa gofu kwa kuiunga mkono timu hiyo wakati wote wa maandalizi.

Mashindano ya Afrika kwa mchezo wa gofu yanafanyikia mjini Accra nchini Ghana kuanzia Agosti 29 hadi Septemba Nne mwaka huu na yanashirikisha timu kutoka mataifa 26.