Manchester City yasema safari yake haijakamilika

0
2362

Mwenyekiti wa klabu ya Manchester City ya nchini England, – Khaldoon Al Mubarak amesema kuwa safari ya klabu hiyo bado haijakamilika licha ya kutoa taarifa ya mapato ya klabu hiyo yenye faida ya Pauni Milioni 500 kwa msimu uliopita.

Taarifa ya iliyotolewa na klabu hiyo imesema kuwa hadi kufikia June 30 mwaka huu, klabu hiyo imetengeza faida ya Pauni Milioni 500 zinazoifanya City kuwa klabu ya pili kwenye ligi ya England nyuma ya Manchester United kuweka rekodi ya kutengeza kiasi kikubwa cha fedha.
Taarifa hiyo pia inaonyesha kuwa huu ni msimu wa Nne mfululizo klabu hiyo inatengeneza faida ambapo kwa mwaka huu imepata faida ya Pauni Milioni 10.4 huku mapato yatokanayo na mishahara ikiwa ni asilimia 52.

Taarifa hiyo inakuja ikiwa miezi minne imepita tangu Man City watwae taji la ligi ya England wakiwa timu ya kwanza kuweka rekodi ya kuvuna alama 100 na Al Mubarak amesema kuwa safari haijakamilika kwa kuwa wana malengo makubwa zaidi huku wakihitajika kufanya vizuri kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya.

Real Madrid, Barcelona, Bayern Munich na Manchester United ndiyo vilabu vinavyotengeneza faida kubwa duniani kuliko Man City ambao wameongeza ukubwa wa uwanja wao wa Etihad kufikia uwezo wa kubebea watazamaji Elfu 55.