Manchester City mbabe kwa Man U

0
1686

Manchester City imeibuka kidedea mbele ya wapinzani wao wa mji mmoja Manchester United kwa mabao matatu kwa moja kwenye mchezo wa ligi kuu ya England.

Magoli ya Manchester City yametiwa kimiani na David Silva, Sergio Kun Aguero na Iga Gundogan na lile ya kufutia machozi la Manchester United limefungwa na Anthon Martial.

Katika michezo mingine, Liverpool imepata ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya Fulham huku Chelsea ikitoka sare ya bila kufungana na Everton.

Arsenal yenyewe imetoka sare ya bao moja kwa moja na Wolverhampton Wanderers.