Liverpool yatolewa kombe la Fa

0
931

Baada ya timu ya Liverool kutolewa katika mzunguko huo wa tatu wa michuano ya FA,  droo ya mzunguko wa nne imeshapangwa ambapo Arsenal wataanzia nyumbani katika dimba lao la Emirates kuwakabili Manchester United.

Vijana hao wa The Gunners wametwaa mara 13 ubingwa wa kombe la FA, huku Manchester United wakitwaa taji hilo mara 12.

Michezo mingine ambayo inatolewa macho na wapenzi wa soka ni Tottenham hotspur, watakaokuwa ugenini kuikabili Crystal Palace, Manchester City   wao watakuwa nyumbani dhidi ya  Burnley  wakati Chelsea  watakuwa katika dimba lao la Stamford Bridge jijini London, kuwakabili Sheffield Wednesday baada ya timu hizo kupambana na kupatika mshindi siku ya jumatano.