Lahyani asimamishwa kuchezesha tenisi

0
2178

Muamuzi wa mchezo wa tenisi Mohamed Lahyani raia wa Sweden amesimamishwa kuchezesha mashindano mawili yajayo ya China Open na Shanghai Masters yatakayofanyika mwezi Oktoba mwaka huu baada ya kupatikana na kosa la kumsaidia mcheza Tenisi,-Kick Kyrgios wa Australia kwenye mashindano yaliyopita ya US Open.

Lahyani alisikika wakati wa mapumziko akimwambia Kyrgios kuwa nataka kukusaidia wakati wa mpambano wake na Pierre – Hugues Herbert wa Ufaransa na baada ya kauli hiyo Kyrgios aliweza kutoka nyuma hadi kuibuka mshindi.

Waandaaji wa mashindano ya US Open wamemtuhumu muamuzi huyo kwa kusema kuwa alienda kinyume na taratibu za mashindano hayo, lakini wamempa tena nafasi ya kuchezesha kwenye mashindano hayo mwaka 2019.

Lahyani atakuwa huru kuchezesha tena mashindano ya tenisi kuanzia mashindano ya Stockholm Open.