Kocha wa Chelsea awalalamikia waamuzi England

0
960

Kocha wa Chelsea Maurizio Sarri amesema, marefa wa England bado hawajui kuitumia technologia ya var katika kuamua mchezo baada ya kutoa penati kwa Tottenham Spurs katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la ligi,mchezo uliochezwa katika uwanja wa wembely na spurs kuibuka na ushindi wa bao moja kwa bila.

Sarri amesema picha za marudio ya video zinaonyesha Harry Kane alikuwa ameotea lakini cha kushangaza mwamuzi wa mchezo ametoa adhabu ya penati aliyofungwa na Kane.

Timu hizo zitakutana katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya pili ya kuwania kombe la ligi, utakaochezwa katika dimba la Stanford Bridge wiki mbili zijazo.