Klabu ya Tottenham kuanza kutumia uwanja wao hivi karibuni

0
869

Klabu ya Tottenham hotspur imesema uwanja wao mpya wa Whitehart Lane utakuwa tayari na kuanza kutumika kwa michezo mbalimbali  kuanzia mwezi wa tatu mwaka huu.

Spur walipanga kuanza kuutumia uwanja wao mpya kuanzia mwezi wa Tisa kufuatia makubaliano ya awali na mkandarasi, lakini ujenzi umeshindwa kukamilika katika muda waliopanga.

Mwenyekiti wa klabu hiyo  Daniel Levy ameomba radhi kwa mashabiki wa timu hiyo kwa kushindwa kuutumia uwanja wao mpya katika muda waliopanga, na sasa wataendelea kuutumia uwanja wa Wembley kama uwanja wao wa nyumbani.