Kaneria akiri kufanya udanganyifu michezoni

0
2149

Mcheza Kriketi maarufu wa Kimataifa raia wa Pakistan, – Danish Kaneria amekiri kuwa alikuwa akitumia udanganyifu wakati wa mchezo huo na kuisababishia timu yake ushindi.

Kaneria amewaomba radhi Raia wa Pakistan na wapenzi wa mchezo wa Kriketi kwa udanganyifu huo ingawa kwa muda wa miaka Sita amekuwa akikanusha kuhusika na tukio hilo.

Kaneria alifungiwa kucheza mchezo wa kriketi miaka Sita iliyopita lakini amekiri makosa yake baada ya kuwa na mahojiano na kituo cha televisheni cha Al Jazeera.