Hazard aiweka njia panda Chelsea

0
1996

Nyota wa klabu ya Chelsea na timu ya Taifa ya Ubelgiji, – Eden Hazard amesema kuwa bado hana uhakika na mustakabali wake ndani ya klabu ya Chelsea kwa kuwa kujiunga na Real Madrid ni ndoto inayosumbua kichwa chake.

Nyota huyo ambaye amebakiza miaka miwili kwenye mkataba wake wa sasa na klabu hiyo ya London amesema kuwa anaogopa kuahidi kama ataongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia Chelsea halafu mwisho wa siku asiongeze.

Hazard mwenye umri wa miaka 27 alihusishwa kuihama Chelsea kwenye dirisha la usajili lililopita ambapo alinukuliwa akisema ana hamu ya kujaribu jambo jipya.

Pamoja na nia hiyo ya Hazard, timu yake bado inataka kumpa mkataba wa muda mrefu mchezaji huyo huku mwenyewe akionekana kulikwepa jambo hilo.

Hazard amenukuliwa akisema kuwa hataki kudanganya kuwa Real Madrid ni timu kubwa na kuongeza kuwa ni timu ya ndoto yake tangu akiwa mtoto.