FIFA kuongeza idadi ya wanawake wanaocheza Soka

0
1877

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) linataka hadi ifikapo mwaka 2026 wanawake milioni sitini wawe wanacheza mpira wa miguu duniani kote.

Katika kuhakikisha suala hilo linafanikiwa, FIFA imepanga kuanzisha mashindano mapya ya soka kwa wanawake ya klabu bingwa ya Dunia kama ilivyo ile ya klabu bingwa ya dunia ya wanaume iliyoanzishwa mwaka 2000.

Hiyo ni sehemu ya mipango ya FIFA katika kuboresha soka la wanawake duniani kote,  ambapo mashindano hayo mapya ni sehemu ya tathmini ya FIFA katika kuboresha soka la wanawake.

Katibu Mkuu wa FIFA, Fatma Samba Diouf Samoura ambaye ni mwanamke wa kwanza kuongoza shirikisho hilo amesema kuwa  amejisikia faraja kuzinduliwa kwa mpango huo na kwamba watakuwa karibu na wanachama wao wote ili kuhakikisha mpango huo unafanikiwa