Everton yaibuka na ushindi dhidi ya Bournemouth

0
870

Timu ya Everton wakiwa nyumbani wameitandika timu ya Bournemouth mabao mawili kwa bila na kusogea hadi nafasi ya kumi katika msimamo wa ligi hiyo.

Mabao ya ushindi ya Everton yamepatikana kipindi cha pili cha mchezo baada ya kumaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza bila majibu.

Mabao hayo yamefungwa na wachezaji Kurt Zouma na Dominic Calvert-Lewin akifunga dakika ya tisini ya mchezo.