BONDIA ALIEMPIGA MZUNGU ASEMA BADO ANASAKA MAFANIKIO

0
1979

Bondia Mtanzania, Hassan Mwakinyo alieshinda pambano lake huko nchini Uingereza dhidi ya Bondia, Sam Eggington amesema kiu yake ya mafanikio ndio imnayomfanya afanye vizuri kwenye pambano hilo.

Akizungumza na TBC toka jijini Birmingham nchini Uingereza, Hassan Mwakinyo amesema siku  zote yeye ni mtu wa kujituma na anataka kufanikiwa na ndio maana alipopata nafasi hiyo ya kwenda kucheza pambano hilo akajianda vizuri na kutotaka kuipoteza nafasi hiyo.

Meneja wa bondia huyo Rashid Nassoro amesema mteja wake alipata nafasi hiyo ya kwenda kucheza pambano nchini Uingereza baada ya mapromoto wa ngumi kumuona bondia wake kupitia mtandao.

Bondia huyo alimpiga bondia Muingereza, Sam Eggington kwenye raundi la pili ya pambano hilo na kumtengenezea sifa kem kem kwa watanzania na wapenda masumbwi kwa ujumla.