Bao la Samatta laipa ushindi Genk

0
2164

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mbwana Samatta amefunga bao la pili katika ushindi wa mabao mawili kwa bila waliopata timu ya Genk dhidi ya Malmo FC huko nchini Ubelgiji.

Leandro Trossad alianza kuifungia Genk bao la kwanza katika dakika ya 37 kabla ya Samatta kuihakikishia ushindi katika dakika ya 71 kwa kupachika bao la pili na kuzima matumaini ya Malmo ya kupata walau alama moja ya ugenini.

Katika matokeo mengine ya ligi ya Yuropa, Sevilla wameitandika Standard Lieg mabao matano kwa moja, Ludogorets wamepokea kipigo cha mabao matatu kwa mawili kutoka kwa Bayer 04 Leverkusen na Dinamo Zagreb wenyewe wameinyuka Fenerbahce mabao manne kwa moja.

Nao Olyimpic Marseile wamekiona cha moto nyumbani baada ya kutandikwa mabao mawili kwa moja na Eintraincht Frankfurt