Aziz K, Saido waitwa timu za Taifa

0
1398

Kiungo wa Yanga na Burkina Faso, Stephane Aziz Ki amejumuishwa katika safu ya viungo saba wanaounda kikosi cha wachezaji 24 wa timu ya Taifa ya nchi hiyo.

Burkina Faso inaingia kambini kujiandaa na mchezo wa kundi B kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2023) dhidi ya Togo ambayo itapigwa Machi 24, 2023.

Wakati huo huo, kiungo wa Simba na Burundi, Saidi Ntibanzonkiza naye ameitwa kambini kujiandaa na mashindano hayo.

Intamba mu Rugamba itashuka dimbani katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Kenya na Indonesia.