Waziri Mkuu kuanza ziara Kagera

0
2642

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Oktoba Sita mwaka huu anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya  siku nne mkoani Kagera.

Akiwa mkoani humo, Waziri Mkuu Majaliwa atatembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo zile za kilimo, afya, elimu na viwanda.

Taarifa iliyotolewa na mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti imewataka wakazi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kumpokea kiongozi huyo.

Wakati wa ziara yake mkoani Kagera, Waziri Mkuu Majaliwa atatembelea wilaya za Bukoba, Kyerwa, Karagwe, Muleba na Biharamulo.