Waziri Mkuu asisitiza ushirikiano kwa ajili ya amani

0
1801

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ushirikiano baina ya taasisi za dini nchini na serikali ni jambo muhimu katika kuimarisha amani.

Waziri Mkuu ameyasema hayo mjini Mwanza akiwa njiani kwenda mkoani Simiyu ambako kesho anatarajia kufungua maonesho ya wajasiriamali.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Mwanza ina wajibu wa kuhakikisha maeneo ya mkoa huo yanaendelea kuwa salama.

Halkadhalika Waziri Mkuu amempongeza Kaimu Sheikh wa mkoa wa Mwanza, Sheikh Hassan Bin Mussa Kabeke kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo.