Watumishi wa afya watakiwa kuendelea kufanya kazi

0
2081

Serikali imewataka watumishi wa sekta ya afya nchini kuendelea kufanyakazi ya kuwatumikia Watanzania kwa upendo wakati ikiendelea kushughulikia matatizo yao mbalimbali.

 

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Rais John  Magufuli katika  hospitali ya wilaya Meatu mkoani Simiyu ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani humo yenye lengo la kukagua na kuzindua miradi mbalimbali pamoja na kuzungumza na wakazi wa mkoa huo.

 

Amesema kuwa serikali kwa upande wake inaendelea kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ya watumishi hao wa sekta ya afya nchini ikiwa ni pamoja na kuongeza vitendeakazi  na kuongeza watumishi zaidi.

 

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, serikali pia italipa madai yote halali wanayodai watumishi hao wa sekta ya afya nchini.

 

Akiwa katika hospitali hiyo ya wilaya ya Meatu, Rais Magufuli pia amewashukuru wadau wote wa sekta ya afya ambao wamekua wakishirikiana na serikali katika kusogeza karibu na Wananchi huduma bora za afya.

 

Rais Magufuli bado anaendelea na ziara yake katika mkoa huo wa Simiyu.