Watu maarufu kutangaza Utalii

0
201

Serikali imeanza mpango wa kuwatumia Wanamichezo na watu maarufu kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo  nchini, ili kuongea idadi ya Watalii wanaotembelea Tanzania.

Akizungumzia ziara ya mchezaji maarufu wa klabu ya Crystal Palace ya nchini Uingereza, – Mamadou Sakho ambaye ni raia wa Ufaransa, Waziri wa Maliasili na utalii Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa, mpango huo umeanza kuonesha mafanikio makubwa.