Watoto washinikiza uchunguzi kifo cha mwenzao

0
2389

Watoto wa shule ya msingi Kibeta katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wamegoma kuingia darasani wakishiniza uchunguzi ufanyike kubaini chanzo cha kifo cha mwanafunzi mwenzao wa darasa la tano Spelius Eradius aliyefariki dunia muda mfupi baada ya kupewa adhabu ya viboko.

Mtoto huyo alipewa adhabu na mmoja wa walimu shuleni hapo akituhumiwa kuiba pochi ya mwalimu.

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Augustino Ollomi amesema mwalimu anayedaiwa kumchapa mtoto huyo anashikiliwa na polisi kwa sababu za kiusalama na uchunguzi zaidi wa tukio hilo.

Kamanda Ollomi alifika katika shule ya msingi Kibeta na kuwatuliza wazazi na watoto ambao hatimaye walikubali kuendelea na masomo.