Watoto waaswa kuwa wazalendo na wenye heshima kwa wazazi wao

0
1100

Mkurugenzi mkuu wa shirika la utangazaji Tanzania Tbc Dakta  Ayub Rioba amewaasa watoto kuwatii na kuwaheshimu walezi na wazazi wao ili Taifa liwe na kizazi chenye uzalendo kwa taifa lao.

Dakta Rrioba ameyasema hayo kwa njia ya simu alipokuwa akitoa salamu za kristmass kwa watoto waliokuwa katika kipindi cha watoto na kristmass kilichorushwa na Tbc taifa na kusema kuwa iwapo watoto wakizingatia mafundisho wanayopewa na walezi na wazazi wao taifa litakuwa na viongozi wazuri wa baadae.

Dakta Rioba pia amewakumbusha wazazi na walezi kutimiza wajibu wao katika malezi ili kuwezesha Taifa kuwa na viongozi watakao fuata nyayo za Rais dakta John Magufuli ya kuonyesha dira ya maisha ya kesho.

Amesema Rais Dakta John Magufuli amedhibiti vitendo visivyofaa na kutokomeza rushwa, vitendo vya wizi na kufanya taifa liwe na watu waadilifu pamoja na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kuboresha miundombinu mbalimbali.