Watoto wa familia moja wauawa kikatili Kagera

0
2102

Miili ya watoto wawili ambao ni ndugu wa familia moja imeokotwa ikiwa imetenganishwa kichwa na kiwiliwili katika shamba la migomba  kwenye kijiji cha Mashule kata ya Kyamulaile wilayani Bukoba mkoani Kagera.

Kufuatia tukio hilo,  Mkuu wa wilaya ya Bukoba, –  Deodatus Kinawiro ameliagiza Jeshi la polisi  wilayani Bukoba kufanya uchunguzi wa haraka na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo.

Watoto hao waliouawa ni Auson Respicius mwenye umri wa miaka Saba na ndugu yake Aristidia Respicius mwenye umri wa miaka Mitano.

Tayari ya jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashilikia watu tisa kwa kuhusika na tukio hilo ambalo linahusishwa na imani za kishirikina.