Watanzania watakiwa kuthamini Lugha ya Kiswahili

0
1106

Rais Dkt John Magufuli amewataka Watanzania kuthamini lugha ya Kiswahili kwani ndio lugha inayomtambulisha duniani.

Akizungumza katika hafla ya  uzinduzi wa ndege mpya aina ya Air Bus 220-300 iliyowasili leo katika  uwanja wa ndege wa zamani Terminal One jijini Dar es salaam Rais Dakta Magufuli  amesema anashangazwa na tabia ya baadhi ya watanzania wanaoona aibu kuzungumza lugha ya Kiswahili huku wakithamini lugha nyingine za nje.

Rais Dakta Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akimsifia  balozi wa Canada nchini  Pamela O”DonnellTanzania ambaye amesoma risala yake kwa lugha ya Kiswahili.

“Ninawashangaa sana watanzania ambao wanaona aibu kuzungumza Kiswahili na ambao wanazungumza na watoto wao kiingereza badala ya kuzungumza nao lugha ya Kiswahili au lugha za asili? Alisema Rais Mgaufuli.

Rais Dakta Magufuli amesema Kiswahili kwa sasa ni lugha ya kumi katika lugha zinazozungumzwa zaidi duniani na raia kutoka nchi mbali mbali wanaendelea kujifunza.