Wasira na Limbu wateuliwa

0
2245

Rais John Magufuli amemteua Stephen Wasira kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Wasira anachukua nafasi ya Profesa Mark Mwandosya.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Dkt Festus Limbu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Dkt Limbu anachukua nafasi ya Dkt John Jingu ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Uteuzi wa viongozi hao umeanza Septemba Tisa mwaka huu.