Wasifu wa JPM: Maisha yake

0
499

Imetimia takribani miaka 5 sasa tangu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli apewe dhamana ya kuliongoza Taifa la Tanzania

Dkt John Pombe Magufuli alizaliwa Oktoba 29 mwaka 1959 katika kijiji cha Chato wilayani Biharamulo Mkoa wa Kagera , hivi sasa Chato ni Wilaya katika Mkoa wa Geita

Dkt John Pombe Magufuli ni Daktari wa Falsafa (PhD) ya kemia, ana mke na Watoto 7

Katika Kipindi cha Miaka 5 ya Uongozi wake Rais Dkt John Magufuli amedhihirisha sifa zote muhimu za Uongozi Bora ameonesha Dira maono na malengo kuhusu mwelekeo wa Taifa la Tanzania

Rais Magufuli wakati wote kiu yake kubwa imekuwa ni kujenga Taifa linalojitegemea katika nyanja zote kisiasa kiuchumi na kijamii.