Wananchi wa Bariadi waaswa kuchemsha maji ya kunywa

0
1396

Wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wameaswa kuwa na utamaduni wa kuchemsha maji ya kunywa ili kuepuka magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu, homa ya tumbo na minyoo.

Hayo yamesemwa na Afisa Afya wa Wilaya ya Bariadi Jumanne Kisanka wakati wa mkutano na watendaji wa vijiji na madiwani wa Tarafa ya Dutwa.

Kisanka amesema visima vingi vya maji havifunikwi na wengine wanachota maji kwenye mito bila kujali usalama wa maji hayo ambapo amewaomba wananchi kuchukua tahadhari ya kuchemsha maji kabla ya kuyanywa.

Katika hatua nyingine Kisaka amewataka viongozi hao kuhakikisha shule zote za msingi katika eneo hilo zina matundu ya vyoo na kwamba shule ambazo hazitakuwa na vyoo vya kutosha zitafungwa.