Wamiliki wa mitandao ya kijamii watakiwa kuwa weledi

0
834

 Mamlaka  ya  mawasiliano  Tanzania  Tcra  nyanda  za  juu  kusini  imewataka  wamiliki wa mitandao  ya kijamii nchini  kufanya kazi  hizo  kwa  kuzingatia  sheria na weledi  katika kutoa habari kwa  jamii.

Wito  huo  umetolewa Mjini Mbeya   na mkuu wa Tcra  kanda  ya nyanda  za  juu kusini, mhandisi  Asajile John mara  baada ya kukutana  na wamiliki wa  mitandao  hiyo mkoani Mbeya.

Ameeleza kuwa mafunzo haya ni sehemu ya  kuwakumbusha wadau hao juu ya   sheria  na taratibu za Tcra katika kutimiza majukumu yao.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kampuni  ya Kukaja ambao  ndio wasimamizi wa mitandao  hiyo anawataka vijana kutumia mawasiliano ya mitandao  kwa njia iliyo sahihi.