Walalamikia Bwawa kutotoa maji

0
2609

Zaidi ya wakulima Elfu 25 wa kata tatu za Igurusi, Ruhanga na Itamboleo wilayani Mbarali mkoani Mbeya wameiomba serikali kuingilia kati mradi wa bwawa la umwagiliaji maji la Rwanyo ambalo tangu kukamilika kwake mwaka 2013 halijawahi kutoa maji.

Wakizungumza na Mwandishi wa TBC mkoani Mbeya, wakulima hao wamedai kuwa pamoja na kwamba ujenzi wa bwawa hilo umegharimu zaidi ya shilingi Bilioni 4.9 hadi kukamilika kwake, bado uwepo wa bwawa hilo haujawanufaisha.

Wakulima wa kata hizo tatu za Igurusi, Ruhanga na Itamboleo wilayani Mbarali mkoani Mbeya wameongeza kuwa matumaini yao ni kuona bwawa hilo linawasaidia katika kuinua sekta ya kilimo, lakini kutokana na kushindwa kutoa maji matumaini hayo hayapo kwa sasa.

Naye msimamizi wa mradi huo wa bwawa la umwagiliaji maji la Rwanyo,- Pius Mwaigonjola amekiri ujenzi wa mradi huo kufanyika chini ya kiwango na hivyo kutokua na uwezo wa kutoa maji