Wakazi wa Rorya waomba wadau kuwachangia ujenzi wa zahanati

0
1031

Wakazi wa Kijiji cha Dett Kata ya Nyaburogo Wilayani Rorya Mkoani Mara wameiomba serikali pamoja na wadau wa maendeleo kuunga mkono jitihada zao ili kufanikisha ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.

Wakazi hao wametoa ombi hilo kufuatia kukwama kwa ujenzi wa zahanati yao kwenye hatua ya kuezeka  ambapo Mbunge wa Rorya Lameck Airo amewataka wasikate tamaa na badala yake waendelee kuchangia ujenzi huo ili kusogeza huduma za afya karibu.

Hadi kufikia sasa ujenzi huo shilingi milioni 15 ambayo ni michango ya wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa Rorya ameendesha harambee ya ujenzi huo na kufikisha kiasi cha shilingi milioni 12.